Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia kupangua makatibu wakuu
Habari za Siasa

Rais Samia kupangua makatibu wakuu

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema, atafanya mabadiliko ya makatibu wakuu wa wizara mbalimbali hivi karibuni. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Amedokeza hilo leo Alhamisi tarehe 1 Aprili 2021, Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, mara baada ya kumaliza kuwaapisha mawaziri, naibu mawaziri na katibu mkuu kiongozi waliowateua jana Jumatano.

Akianza kuzungumza kwa kuwasalimia viongozi mbalimbali waliohudhulia hafla hiyo, Rais Samia aliuliza makatibu wakuu mpo, heloooo…kisha wakasimama kumsalimia naye akasema mmetulia ninyi “siyo leo lakini nakuja.”

Mara baada ya kumaliza hotuba yake fupi, Rais Samia akizungumzia sikukuu ya Pasaka akisema kuanzia kesho Ijumaa hadi Jumatatu ni sikuu “tutakutana hapa Jumanne” kushuhudia wengine wakiapishwa.

Hata hivyo, Rais Samia hakusema hasa hiyo Jumanne, watakaoapishwa watakuwa makatibu wakuu au wengine, kama wakuu wa mikoa, wilaya au makatibu tawala wa mikoa.

Rais Samia amewaonya wateule wake, watakaokuwa wakipandisha mabega akisema “nitakuwa na kipimo cha mabega, nikiona mtu anapandisha mabega nitaona huyu si mtumishi wa wananchi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!