Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mama Samia kuapishwa leo
Habari za Siasa

Mama Samia kuapishwa leo

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

LEO Ijumaa saa 4:00 asubuhi, tarehe 19 Machi 2021, Ikulu ya Dar es Salaam, Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, ataapishwa kuwa Rais wa sita wa Tanzania katika awamu ya tano. Anaripoti Hamis Mguta…(endelea).

Mama Samia anaapishwa kuhitimisha awamu ya tano ya uongozi wa miaka minne na ushehe iliyosalia, baada ya Rais John Pombe Magufuli (61), kufariki dunia.

Rais Magufuli alifariki dunia Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021 katika Hospitali ya Mzena, Makumbusho mkoani Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo.

Mama Samia, mwenye umri wa miaka 61, anatarajiwa mara baada ya kumaliza kuapishwa, kutangaza ratiba ya mazishi ya Rais Magufuli ambaye atazikwa nyumbani kwao Chato mkoani Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!