Thursday , 30 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe amtwisha mzigo Mama Samia
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe amtwisha mzigo Mama Samia

Spread the love

 

MWENYEKITI wa chama kikuu cha upinzani Tanzania- Chadema, Freeman Mbowe amemtumia salamu Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kufuatilia kifo cha Rais John Pombe Magufuli (61). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Rais Magufuli, alifikwa na mauti saa 12 jioni ya Jumatano tarehe 17 Machi 2021, Hospitali ya Mzena, Makumbusho, mkoani Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo wake.

 

Mama Samia, ametangaza siku 14 za maombolezo na bendera zitapepea nusu mlingoti huku taratibu za mazishi zitatolewa baadaye.

Katika salamu hizo ambazo amezitoa Mbowe, ametoa pole kwa Mama Samia ambaye ataapishwa wakati wowote kuwa Rais, Janeth, Mjane wa Rais Magufuli, familia na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Pamoja na kuwa katika wakati wa majonzi na maombolezo ya kitaifa, kifo hiki kinatukumbusha na kutufundisha thamani ya maisha na utu wetu na kuwa na upendo katika kutenda yaliyo mema wakati wa uhai wetu hapa duniani,” amesema Mbowe

Amesema, kipindi hiki cha maombolezo, “tukitumie kufungua ukurasa mpya wa kulirejesha taifa kuwa moja na lenye kulinda na kuheshimu uhuru, haki, utawala wa sheria, demokrasia na maendeleo ya watu.”

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan

Mbowe amesema,”ni imani yetu, kuwa Rais ajaye, Mama Samia atalinda misingi hiyo na ataliongoza Taifa kufikia maridhiano ya Kitaifa.”

“Tuna amini, Samia alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba, atalipatia Taifa katiba mpya iliyotokana na maoni ya wananchi.”

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!