Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbowe amtwisha mzigo Mama Samia
Habari za SiasaTangulizi

Mbowe amtwisha mzigo Mama Samia

Spread the love

 

MWENYEKITI wa chama kikuu cha upinzani Tanzania- Chadema, Freeman Mbowe amemtumia salamu Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan kufuatilia kifo cha Rais John Pombe Magufuli (61). Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea).

Rais Magufuli, alifikwa na mauti saa 12 jioni ya Jumatano tarehe 17 Machi 2021, Hospitali ya Mzena, Makumbusho, mkoani Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya mfumo wa umeme wa moyo wake.

 

Mama Samia, ametangaza siku 14 za maombolezo na bendera zitapepea nusu mlingoti huku taratibu za mazishi zitatolewa baadaye.

Katika salamu hizo ambazo amezitoa Mbowe, ametoa pole kwa Mama Samia ambaye ataapishwa wakati wowote kuwa Rais, Janeth, Mjane wa Rais Magufuli, familia na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

“Pamoja na kuwa katika wakati wa majonzi na maombolezo ya kitaifa, kifo hiki kinatukumbusha na kutufundisha thamani ya maisha na utu wetu na kuwa na upendo katika kutenda yaliyo mema wakati wa uhai wetu hapa duniani,” amesema Mbowe

Amesema, kipindi hiki cha maombolezo, “tukitumie kufungua ukurasa mpya wa kulirejesha taifa kuwa moja na lenye kulinda na kuheshimu uhuru, haki, utawala wa sheria, demokrasia na maendeleo ya watu.”

Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan

Mbowe amesema,”ni imani yetu, kuwa Rais ajaye, Mama Samia atalinda misingi hiyo na ataliongoza Taifa kufikia maridhiano ya Kitaifa.”

“Tuna amini, Samia alikuwa makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba, atalipatia Taifa katiba mpya iliyotokana na maoni ya wananchi.”

3 Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!