Saturday , 18 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba yamfukuzisha Kaze Yanga
MichezoTangulizi

Simba yamfukuzisha Kaze Yanga

Cedric Kaze, Kocha wa Yanga
Spread the love

 

MCHEZAJI wa zamani wa klabu ya Yanga, Ally Mayai amesema ubora wa kikosi cha Simba kwa sasa umechangia na kusukua, uongozi wa Yanga kumtimua kazi kocha wake, Cedric Kaze raia wa Burundi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Yanga ilifikia maamuzi ya kumfukuzisha kazi kocha huyo ambaye amedumu ndani ya kikosi hiko kwa siku 139 toka alipokuja nchini kufuatia matokeo mabovu waliopata kwenye mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Tanzania bara.

MwanaHALISI Online ilimtafuta Ally Mayai mchezaji wa zamani wa klabu hiyo ambaye alicheza kwa mafanikio alieleza kuwa kama Simba isingekuwa kwenye ubora na nafasi hii waliopo huwenda Yanga wasingemfukuza Kaze.

“Kama Simba isingekuwa kwenye nafasi ile, labda ingekuwa kwenye nafasi ya tisa, pengine Cedric Kaze asingefukuzwa na kusingekuwa na presha yoyote kutoka kwa mashabiki na wanachama.

“Simba kama leo hii akishinda mechi zake zote alizokuwa nazo mkononi ataiacha Yanga kwa pointi saba ndiyo sababu iliyopelekea uongozi kuondoa benchi la ufundi mara baada ya kuona kiwango cha timu kinashuka,” alisema Mayai.

Aidha Mayai aliongezea kwa kusema kuwa uwekezaji walioufanya Yanga hauendani na kiwango kinachoonekana uwanjani na hata matokeo pia kwenye michezo ya hivi karibuni.

“Yanga ilionekana kuwa na mapungufu mengi uwanjani, kiwango cha uwekezaji uliofanyika hakiakisi na matokeo ya uwanjani, kwa mfano ile mechi ya Yanga na Kengold hakukuwa na tofauti kubwa sana kati ya timu zote mbili, wakati uwekezaji uliowekezwa alitakiwa mtu aone hii ni Yanga na hii ni Kengold ambao wapo daraja la kwanza,” aliongezea mchezaji huyo wa zamani.

Uongozi wa timu hiyo umemtimua kocha huyo pamoja na benchi lake lote la ufundi huku ikiwa kileleni kwenye msimamo wakiwa na pointi 50, baada ya kucheza michezo 23, huku wapinzani wao klabu ya Simba wakiwa kwenye nafasi ya pili wakiwa na pointi 45, na michezo 19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

Habari za SiasaTangulizi

Haya hapa majina walioteuliwa kugombea nafasi mbalimbali CHADEMA

Spread the loveCHAGUZI wa kanda za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Uingereza yamwaga bil. 9 kumuunga mkono Samia matumizi nishati

Spread the loveWaziri Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Selemani...

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe abadili mbinu ya kudai Katiba mpya

Spread the loveMwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (Chadema), Fremaan Mbowe amebadili mbinu...

error: Content is protected !!