Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Jiji Dodoma laonya machinga
Habari Mchanganyiko

Jiji Dodoma laonya machinga

Afisa masoko wa jiji la Dodoma James Yuna akiwaondoa wafanyabiashara wanaopanga biashara zao kwenye maeneo hatarishi ya kiafya katika soko la Sabasaba
Spread the love

JAMES Yuna, Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, amewataka wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) kuacha kufanya biashara kwenye maeneo yasiyo rasmi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 2 Februari 2021, wakati akiwaelimisha baadhi ya wafanyabiashara hao waliopanga bidhaa zao sehemu za waenda kwa miguu ikiwemo kwenye madaraja.

Amesema, baadhi ya madaraja hayo yaliyopo ndani ya jiji hilo, yamevamiwa na wamachinga kwa kuweka bidhaa mbalimbali bila kujali maana halisi ya matumizi yaliyokusudiwa na mipango miji.

“Niombe tuheshimu matumizi ya madaraja haya ambayo serikali yameyajenga ili kuwarahisisha watembea kwa miguu kupita sehemu salama, kwa maana hiyo ninahitaji yawe wazi na sivyo vinginevyo,” amesema.

Pia, amewataka mamalishe ndani ya masoko kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya kwa kuweka vyombo vya kunawa na sabuni, ili kujikinga na magonjwa mbalimbali ya maambukizo.

Akizungumza na mama lishe wa Soko Kuu la Majengo, jijini Dodoma amesema, wanatakiwa kuchukua tahadhali ya magonjwa ya maambukizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

GGML, OSHA wawanoa mama lishe 50 kukabiliana na majanga ya moto

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!