Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Jiji Dodoma laonya machinga
Habari Mchanganyiko

Jiji Dodoma laonya machinga

Afisa masoko wa jiji la Dodoma James Yuna akiwaondoa wafanyabiashara wanaopanga biashara zao kwenye maeneo hatarishi ya kiafya katika soko la Sabasaba
Spread the love

JAMES Yuna, Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, amewataka wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) kuacha kufanya biashara kwenye maeneo yasiyo rasmi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 2 Februari 2021, wakati akiwaelimisha baadhi ya wafanyabiashara hao waliopanga bidhaa zao sehemu za waenda kwa miguu ikiwemo kwenye madaraja.

Amesema, baadhi ya madaraja hayo yaliyopo ndani ya jiji hilo, yamevamiwa na wamachinga kwa kuweka bidhaa mbalimbali bila kujali maana halisi ya matumizi yaliyokusudiwa na mipango miji.

“Niombe tuheshimu matumizi ya madaraja haya ambayo serikali yameyajenga ili kuwarahisisha watembea kwa miguu kupita sehemu salama, kwa maana hiyo ninahitaji yawe wazi na sivyo vinginevyo,” amesema.

Pia, amewataka mamalishe ndani ya masoko kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya kwa kuweka vyombo vya kunawa na sabuni, ili kujikinga na magonjwa mbalimbali ya maambukizo.

Akizungumza na mama lishe wa Soko Kuu la Majengo, jijini Dodoma amesema, wanatakiwa kuchukua tahadhali ya magonjwa ya maambukizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mchina wa SGR aburuzwa kortini kwa kumjeruhi Mtanzania, TRC waja juu

Spread the love  RAIA wa China, Zheng Yuan Feng, amefikishwa mahakamani kwa...

Habari Mchanganyiko

Watendaji Kata, Mitaa watakaoshindwa kusimamia usafi kukiona

Spread the love  WATENDAJI wa kata, mitaa na vitongoji na maofisa afya...

Habari Mchanganyiko

Mtia nia urais TLS kukata rufaa kupinga kuenguliwa

Spread the love  MTIA nia ya kugombea Urais wa Chama cha Mawakili...

Habari Mchanganyiko

NBC yazindua kampeni ya mkeka wa ushindi na ATM zake

Spread the loveBENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imetangaza uzinduzi wa kampeni...

error: Content is protected !!