Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Jiji Dodoma laonya machinga
Habari Mchanganyiko

Jiji Dodoma laonya machinga

Afisa masoko wa jiji la Dodoma James Yuna akiwaondoa wafanyabiashara wanaopanga biashara zao kwenye maeneo hatarishi ya kiafya katika soko la Sabasaba
Spread the love

JAMES Yuna, Ofisa Masoko wa Jiji la Dodoma, amewataka wafanyabiashara ndogondogo (wamachinga) kuacha kufanya biashara kwenye maeneo yasiyo rasmi. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Ametoa kauli hiyo leo Jumanne, tarehe 2 Februari 2021, wakati akiwaelimisha baadhi ya wafanyabiashara hao waliopanga bidhaa zao sehemu za waenda kwa miguu ikiwemo kwenye madaraja.

Amesema, baadhi ya madaraja hayo yaliyopo ndani ya jiji hilo, yamevamiwa na wamachinga kwa kuweka bidhaa mbalimbali bila kujali maana halisi ya matumizi yaliyokusudiwa na mipango miji.

“Niombe tuheshimu matumizi ya madaraja haya ambayo serikali yameyajenga ili kuwarahisisha watembea kwa miguu kupita sehemu salama, kwa maana hiyo ninahitaji yawe wazi na sivyo vinginevyo,” amesema.

Pia, amewataka mamalishe ndani ya masoko kufuata maelekezo ya wataalamu wa afya kwa kuweka vyombo vya kunawa na sabuni, ili kujikinga na magonjwa mbalimbali ya maambukizo.

Akizungumza na mama lishe wa Soko Kuu la Majengo, jijini Dodoma amesema, wanatakiwa kuchukua tahadhali ya magonjwa ya maambukizi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!