Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TLS: Mahakama isikubali kupokwa mamlaka
Habari Mchanganyiko

TLS: Mahakama isikubali kupokwa mamlaka

Dk. Rugemeleza Nshala
Spread the love

 

CHAMA cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kimeitaka mahakama “iishi Katiba ya nchi, ilinde mamlaka yake kwa wivu wote na isiruhusu mamlaka yake kupokwa.” Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo Jumatatu tarehe 1 Februari 2021, na rais wa chama hicho, Dk. Rugemeleza Nshalla katika Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini na miaka 100 ya Mahakama Kuu yaliyofanyika kwenye viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma.

Katika hotuba yake, Dk. Nshalla amesema, kucheleweshwa kwa kesi au kuahirishwa kutokana na kuchelewa kwa upelelezi, kumekuwa changamoto ya muda mrefu.

“Kuna watuhumiwa na mahabusu wengi wanaendelea kusota magerezani kwa kisingizio cha upelelezi kutokamilika, hii si sawa hata kidogo,” amesema Dk. Nshalla.

“Muda wa mwanadamu kuishi una ukomo wake, kila siku inayopita hairudi, ukimshika na kumweka ndani na kuendelea kumweka ndani, huna uwezo wa kumfidia muda huo wa uhuru uliomnyang’anya.

“Wewe unayemuweka ndani si Mungu ndiye anatupa uhai, njia pekee ya kuhakikisha unaheshimu uhuru wa mtu ni kuhakikisha upelelezi unapokuwa umekamilika au kama haujakamilika, anapewa dhamana, hivyo makosa yote yadhaminike,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!