Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mchungaji afungwa miaka 140 jela, amlaumu shetani
KimataifaTangulizi

Mchungaji afungwa miaka 140 jela, amlaumu shetani

Mchungaji Boniface Amani Gichina,
Spread the love
BONIFACE Amani Gichina, Mchungaji wa Kanisa la Living Faith Church maarufu Winners’ Chapel International, nchini Kenya amefungwa jela miaka 140 kwa kuwapa mimba mabinti zake wawili. Inaripoti BBC … (endelea).

Anthony Mwicigi, Hakimu Mkuu wa Mahakama ya Baricho nchini humo, amemuhukumu Mchungaji Gichina (51) kwa ubakaji wa watoto wake wenye miaka 14 na 16.

Tayari mabinti zake hao wamejifungua, mmoja akiwa na mtoto wa miezi saba na mwingine miezi mitano.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Anthony amemuhukumu mchungaji huyo kifungo cha miaka 70 kwa kila binti yake, na kueleza hukumu hizo zitatekelezwa moja baada ya nyingine.

Mhungaji Gichina anayetoka katika Kaunti ya Kirinyaga, mbele ya mahakama hiyo, alikiri kubaka watoto wake na kisha kuwajaza mimba.

Mchungaji huyo baada ya kufanya hivyo na kubaini anatafutwa, alitoweka lakini alikamatwa kutokana na msako ulioondeshwa na polisi.

Ameiambia mahakama hiyo, amerubuniwa na shetani na kusababisha kuwaingilia mabinti zake wote na hivyo, anamlaumu kwa kumrubuni na kutenda kosa hilo.

Kutokana na kosa hilo, amewaomba msamaha watoto wake pamoja na mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!