Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Facebook wamnyoosha Museveni, ajibu mapigo
KimataifaTangulizi

Facebook wamnyoosha Museveni, ajibu mapigo

Spread the love

MTANDAO wa kijamii wa Facebook umefungia akaundi zinazoshabikia Chama Tawala cha Uganda, NRM kinachoongozwa na rais wa nchi hiyo, Yoweri Museveni. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Kutokana na hatua hiyo, Rais Museveni na serikali yake wameamua kufungia mitandao yote ya kijamii kuanzia jana tarehe 13 Januari, 2021.

Leo tarehe 14 Januari 2021, Raia wa Uganda wapo kwenye foleni ya kura kwenye uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.

Rais Musemeni amenukuliwa akisema, uamuzi huo unatokana na hatua ya Facebookkufungia akaunti za wafuasi wake.

Yoweri Museveni

Kwenye uchaguzi huo uliotanguliwa na mauaji ya hovyo yaliyofanywa na vikosi vya usalama kwa raia wa nchi hiyo, Rais Museveni anakabiliana na upinzani mkali kutoka kwa Robert Kyagulanyi (Bobi Wine) (38), wanamuziki wa kizazi kipya.

Bobi Wine anatamba kumng’oa Rais Museveni kwa madai ya kuongoza kizazi kipya cha wapiga kura ambao ni wengi nchini Uganda, naye Rais Museveni anayegombea kwa mara ya sita akiwa madarakani kwa miaka 35 sasa, anatamba kustawisha jamii ya Waganda.

Katika kukabiliana na kile kinachoitwa vurugu, Polisi Uganda wameeleza kwamba, maofisa wake watakaa kwenye majengo marefu Kampala, ili kufautilia kila kinachotokea huku wengine wakizunguka mitaani.

Taifa hilo linaingia kwenye uchaguzi ikiwa tayari watu zaidi ya 50 wamepoteza maisha tangu kuanza kwa hekaheka za uchaguzi mkuu nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaTangulizi

Mapya yaibuka wamasai waliohamishwa Ngorongoro kwenda Msomera

Spread the loveMAPYA yameibuka kuhusu zoezi la Serikali kuwahamisha kwa hiari wamasai...

Habari MchanganyikoTangulizi

Baba aomba msaada kuzika miili ya familia yake iliyofunga bila kula kuonana na Mungu

Spread the loveWAKATI Mamlaka nchini Kenya, ikiendelea kukabidhi miili ya watu waliofariki...

Habari za SiasaTangulizi

Makonda awapopoa wanaomtofautisha Magufuli na Samia

Spread the loveKATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM),...

error: Content is protected !!