Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Michezo Beki Yanga apata pigo, afiwa na watu wawili kwa mpigo
Michezo

Beki Yanga apata pigo, afiwa na watu wawili kwa mpigo

Bakari Mwamnyeto
Spread the love

BEKI wa kati na nahodha msaidizi wa klabu ya Yanga, Bakari Mwamnyeto amepata pigo kwa kufiwa na mchumba wake pamoja na mtoto usiku wa kuamkia leo kwenye hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati akijifungua. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Mwamnyeto moja ya wachezaji waliokuwa kambini kwenye kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ ambacho kinajiandaa na michuano ya Kombe la mataifa Afrika kwa wachezaji wa ndani ‘Chan.’

Kwa upande wa Yanga kupitia Afisa Habari na mhamasishaji wa klabu klabu hiyo, Antonio Nugaz katika kuthibitisha taarifa hizo amesema kuwa “bado taratibu za msiba zinafanyika na zitakapokamilika wataweka wazi unafanyika wapi.”

Yanga kupitia kurasa yao ya kwenye mtandao wa Instagram wametuma salamu za rambirambi kwa beki wao huyo pamoja na ndugu, jamaa na marafiki walioguswa na msiba huo.

Kwasasa kikosi cha Yanga kipo visiwani Zanzibar kwenye kombe la Mapinduzi ambapo leo kitashuka dimbani majira ya saa 2:15 kuwakabili Namungo FC kwenye mchezo wa kundi A, utakaopigwa kwenye uwanja wa Amani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!