Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mo Salah aitikisa Liverpool
Habari Mchanganyiko

Mo Salah aitikisa Liverpool

Mohamed Salah
Spread the love

KAULI ya Mohamed Salah, mshambuliaji wa Klabu ya Liverpool kwamba, alifedheheshwa kwa kutopewa nafasi ya unahodha wakati wa mechi yao na Midtjylland, Klabu Bingwa Ulaya imetikisa. Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Salah ambaye ana misimu mine tangu kujiunga na klabu hiyo, anahusishwa na kutaka kukimbilia Hispania na kujiunga na Klabu ya Barcelona ama Real Madrid baada ya kuhisi kuonekana ‘kimeo’ kwenye klabu yake ya sasa.

Katika mechi hiyo iliyopigwa tarehe 9 Desemba 2020, Salaa anasema alitarajia kupangwa na hodha lakini kocha wake hakumpa nafasi hiyo.

“Ukweli nilifedheheshwa sasa, nilitarajia kuwa nahodha, lakini ni uamuzi wa meneja hivyo nakubaliana nao,” alisema Salah wakati wa mahojiano na chombo kimoja cha habari cha Hispania.

Kauli hiyo imeibua mkanganyiko mkubwa miongoni mwa mashabiki wa klabu hiyo, huku taarifa za kutaka kuondoka kwake zikizidi kupamba moto.

Jurgrn Klopp, Kocha wa Liverpool alipoulizwa kuhusu kauli ya Salah, alisema hana cha kuongea.

Amesema, ni mara yake ya kwanza kumsikia Salah akilalamikia hilo “…tulicheza Jumapili na Jumatano kwa hivyo tulihitaji kupumzisha miguu. “Klopp alisema na kuongeza “Mo alikosa dakika saba tu katika michezo minne iliyopita.”

Hata hivyo, tayari klabu yake imeeleza kwamba, haina mpango wa kumwachia mshambuliaji huo mwenye mkataba naye mpaka mwaka 2023.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!