Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Bosi sekretarieti ya maadili afariki, JPM amlilia
Habari za Siasa

Bosi sekretarieti ya maadili afariki, JPM amlilia

Rais John Magufuli
Spread the love

ALIYEKUWA Kamishana wa Sekretarieti ya Maandili ya Viongozi wa Umma nchini Tanzania, Jaji mstaafu Harold Nsekela amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa za kifo chake, zimetolewa leo Jumapili tarehe 6 Desemba 2020 na Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli kupitia akaunti yake ya Twitter.

Hata hivyo, Rais Magufuli hajaeleza, Jaji Nsekela amefikwa na mauti kwa tatizo gani au hospitali aliyokuwa amelazwa.

“Nimesikitishwa na kifo cha Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Harold Nsekela. Poleni familia, watumishi wote wa Sekretarieti ya Maadili na Mahakama.”

“Jaji mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapakazi. Mungu amweke mahali pema, Amina,” amesema Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!