Sunday , 2 April 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Bosi sekretarieti ya maadili afariki, JPM amlilia
Habari za Siasa

Bosi sekretarieti ya maadili afariki, JPM amlilia

Rais John Magufuli
Spread the love

ALIYEKUWA Kamishana wa Sekretarieti ya Maandili ya Viongozi wa Umma nchini Tanzania, Jaji mstaafu Harold Nsekela amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa za kifo chake, zimetolewa leo Jumapili tarehe 6 Desemba 2020 na Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli kupitia akaunti yake ya Twitter.

Hata hivyo, Rais Magufuli hajaeleza, Jaji Nsekela amefikwa na mauti kwa tatizo gani au hospitali aliyokuwa amelazwa.

“Nimesikitishwa na kifo cha Kamishna wa Maadili, Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Harold Nsekela. Poleni familia, watumishi wote wa Sekretarieti ya Maadili na Mahakama.”

“Jaji mstaafu Nsekela alikuwa mwadilifu, mzalendo, asiyejikweza na mchapakazi. Mungu amweke mahali pema, Amina,” amesema Rais Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia apangua mawaziri

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan, amefanya mabadiliko madogo ya Baraza la...

Habari za Siasa

RC mstaafu afariki dunia, CCM yamlilia

Spread the loveALIYEWAHI kuwa mkuu wa mikoa ya Dodoma, Mara, Mtwara na...

Habari za Siasa

Marekani kuwekeza Dola 500 Mil kupeleka bidhaa na huduma Tanzania

Spread the loveMAKAMU wa Rais wa Marekani, Kamala Harris amesema miongoni mwa...

Habari za Siasa

Kamala ataja hatua mpya kuimarisha uhusiano wa kibiashara Tanzania, Marekani

Spread the loveKATIKA kuimaridha uhusiano wa kibiashara na kiuchumi baina ya Tanzania...

error: Content is protected !!