Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Rais Mwinyi kutangza mawaziri kesho
Habari Mchanganyiko

Rais Mwinyi kutangza mawaziri kesho

Dk. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi kesho Alhamisi tarehe 19 Novemba 2020, ataweka wazi sura ya baraza lake jipya la mawaziri. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Dk. Mwinyi ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, atakuwa anaunda baraza hilo la kwanza tangu alipoingia madarakani tarehe 2 Novemba 2020.

Rais Mwinyi aliingia madarakani akichukua nafasi ya mtangulizi wake, Dk. Ali Homahed Shein aliyemaliza miaka kumi ya utawala wake kwa mujibu wa Katiba.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano na Hassan Hassan, Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na Habari, Ikulu imesema, Rais Mwinyi atatangaza baraza hilo, kesho Alhamisi saa 4:00 asubuhi

Taarifa hiyo ya uteuzi, imezidisha presha kwa Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuona nani atateuliwa ili kuanza safari ya miaka mitano ya kuwatumikia Wazanzibar kwenye nafasi watakazoteuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!