Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Wahamiaji 36 wa Ethiopia, Somalia wadakwa Dar
Habari Mchanganyiko

Wahamiaji 36 wa Ethiopia, Somalia wadakwa Dar

Spread the love

WAHAMIAJI haramu 36 raia wa Ethiopia na Somalia walioingia nchini Tanzania kinyume na taratibu, wamekamatwa. Anaripoti Mwandishi Wetu

Wahamiaji hoa wamekamatwa na vyombo vya ulinzi na usalama Mkoa wa Dar es Salaam usiku wa kuamkia Jumapili tarehe 15 Novemba 2020 kwenye fukwe za Mbweni jijini humo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumatano tarehe 18 Novemba 2020, Mkuu wa Mkoa huo (RC), Aboubakar Kunenge, ametoa onyo kali kwa raia wa Tanzania wanaoshiriki kuwafadhili na kuwasafirisha ili wapate fedha.

Kunenge amesema, wahamiaji hao walikamatwa usiku wa kuamkia tarehe 15 Novemba kwenye fukwe za Mbweni ambapo kati yao 30 wanatoka Ethiopia na sita wanatoka Somalia.

Amesema, hata utaratibu unaotumika kusafirisha watu hao unakiuka sheria, haki na utu wa binadamu sababu wengi wao wanafungiwa kwenye kontena zisizokuwa na hewa na pindi wanapobainika kufariki Dunia maiti zao hutupwa kwenye vichaka.

Pia, mkuu huyo wa mkoa, amevipongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya.

Kwa upande wake, Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishina Msaidizi Edmund Mrosso, amesema kinachofuata baada ya wahamiaji hao kukamatwa watafikishwa mahakamani kwa kosa la kuingia nchini kinyume na taratibu.

Aidha Kamishina Mroso amesema, kwa wale wanaowasafirisha au kuwahifadhi wahamihaji hao adhabu inaelekeza kifungo cha miaka 20, faini ya Sh.20 milioni au vyote kwa pamoja ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zilizotumika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!