Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Michezo MO Dewji: Chama kwenda Yanga? ‘tumemaliza naye’
Michezo

MO Dewji: Chama kwenda Yanga? ‘tumemaliza naye’

Mohamed Dewji (MO), Mwekezaji wa klabu ya Simba
Spread the love

MWENYEKITI wa Klabu ya Simba, Mohamed Dewji ‘MO Dewji’ amesema, mchezaji wao, Clatous Chama ataendelea kuhudumu klabuni hapo hadi mwaka 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea)

MO Dewji amesema hayo leo Jumapili tarehe 15 Novemba 2020 wakati anazungumza na waandishi wa habari akitoa mrejesho wa kikao cha bodi ya ligi kilichofanyika jana Jumamosi.

Amesema, kumekuwa na maneno mengi yanayoendelea mitandaoni kuhusu kiungo huyo raia wa Zambia, Chama kujiunga na watani zao, Yanga hali inayoipua presha kwa mashabiki na viongozi wa mabingwa hao watetezi wa ligi kuu ya vodacom Tanzania Bara.

Clatous Chama

“Kumekuwa na kelele nyingi sana kuhusu Chama mara (Meddie) Kagere, sisi Simba tumejipanga na hili la Chama amekwenda sijui Yanga, Chama tumesaini nae mtakana mpaka 2022. Hii hoja ya Chama imeishia hapa,” amesema MO Dewji.

Amesema “Kuna propaganda zinaendelea. Kuna gazeti nimesoma Chama amevaa jezi ya Yanga, ujue tusiende na mambo ya barabarani, sisi Simba hatuwezi kuropoka ropoka hovyo, sisi mambo ya Chama tumekwisha maliza.”

Katika kusisitiza hilo, amesema “Chama tumemalizana naye mapema, hatukutaka kutangaza, lakini hizi propaganda zisizo na maana hazifai.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

error: Content is protected !!