Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madai kura feki, Polisi wamkamata Mdee na kumwachia
Habari za Siasa

Madai kura feki, Polisi wamkamata Mdee na kumwachia

Halima Mdee, aliyekuwa ubunge wa Kawe kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

JESHI la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni asubuhi ya leo Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 walimkata Mgombea Ubunge wa Kawe, Halima Mdee wa Chadema kufuatia sintofahamu iliyojitokeza katika zeozi la upigaji kura jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Taarifa zinaeleza, Mdee alikamatwa katika Kituo cha Kawe kufuatia sintofahamu hiyo kutokea baada ya mgombea huyo kudai kuona masanduku ya kura yakiwa na kura zilizopigwa kinyume na utaratibu.

Akizungumzia sakata hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Edward Bukombe amesema, mgombea huyo alihojiwa baada ya kukamatwa kisha akaachiwa huru.

Kuhusu madai ya Mdee ya sanduku kukutwa na kura za kughushi, Kamanda Bukombe amesema hawajapokea taarifa hizo.

“Mdee yuko huru, kulikuwa na tafrani ikapelekea ahojiwe lakini baadae aliachiwa huru. Chanzo ilikuwa kutoelewana,” amesema

“Kwenye uchaguzi ni kawaida  kuona mtu mabishano,  kulitokea mabishano, ilikuwa ni kituo cha Kawe, bado taarifa za kuwa masanduku yalikuwa na kura bado hatujapokea,” amesema Kamanda Bukombe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!