Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwandishi TBC afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Mwandishi TBC afariki dunia

Spread the love

MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba amesema, Elia amefikwa na mauti leo Jumamosi tarehe 24 Oktoba 2020 alipokuwa amelazwa hospitalini hapo kwa matobabu.

Dk. Rioba amesema,taarifa zaidi zitatolewa.

 

Kwa upande wake, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk. Hassan Abbas, ametumia ukurasa wa Twitter kuomboleza kifo hicho cha Elia.

“Kwa niaba ya Serikali, tumepokea kwa masikitiko kifo cha Mtangazaji mahiri wa TBC, Elisha Elia, kilichotokea leo Dar es Salaam.”

Dk. Abbas ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema,”Elisha atakumbukwa kwa kipaji chake adhimu katika uandishi wa habari za magazeti na baadaye kuwa mtangazaji galacha.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!