Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwandishi TBC afariki dunia
Habari Mchanganyiko

Mwandishi TBC afariki dunia

Spread the love

MWANDISHI wa Habari wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Elisha Elia amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea). 

Mkurugenzi Mkuu wa TBC, Dk. Ayub Rioba amesema, Elia amefikwa na mauti leo Jumamosi tarehe 24 Oktoba 2020 alipokuwa amelazwa hospitalini hapo kwa matobabu.

Dk. Rioba amesema,taarifa zaidi zitatolewa.

 

Kwa upande wake, Msemaji Mkuu wa Serikali ya Tanzania, Dk. Hassan Abbas, ametumia ukurasa wa Twitter kuomboleza kifo hicho cha Elia.

“Kwa niaba ya Serikali, tumepokea kwa masikitiko kifo cha Mtangazaji mahiri wa TBC, Elisha Elia, kilichotokea leo Dar es Salaam.”

Dk. Abbas ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo amesema,”Elisha atakumbukwa kwa kipaji chake adhimu katika uandishi wa habari za magazeti na baadaye kuwa mtangazaji galacha.”

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!