Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aahidi neema wanafunzi elimu ya juu
Habari za Siasa

Lissu aahidi neema wanafunzi elimu ya juu

Spread the love

MGOMBEA Urais wa Tanzania kupitia Chadema, Tundu Lissu amesema, akichaguliwa kuwa Rais wan chi hiyo ataondoa ubaguzi wa utoaji mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu na kupunguza riba wanayolipa kwa sasa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza … (endelea).

Lissu ametoa ahadi hiyo leo Jumamosi tarehe 26 Septemba 2020 alipokuwa akizungumza na wahariri na waandishi wa habari jijini Mwanza kabla ya kuendelea na mikutano yake ya kampeni Mwanza na Mkoa wa Mara.

Uchaguzi Mkuu wa Tanzania utafanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 ukihusisha uchaguzi wa Rais, wabunge na madiwani.

“Hili suala la bodi ya mikopo ya wanafunzi, ilipoanzishwa sheria ya bodi ya mikopo ya wanafunzi wa elimu ya juu, kiwango cha riba kilichowekwa ilikuwa asilimia tatu ya marejesho ya mkopo.”

“Sasa wameondoa asilimia tatu na kupeleka asilimia 15. Sisi tumesema tutarudi katika mkataba wa mwanzo wa asilimia tatu ukipata ajira na kama huna ajira utalipaje hela kwani huna hela,” amesema Lissu

“Wapate ajira na tutakata watape ajira ndani na nje ya nchi ili walipe kwa asilimia tatu na tutaondoa ubaguzi kabisa katika utoaji wa mikopo.”

Lissu amesema “kwa sasa ukisoma shule binafsi hupati mkopo, kila Mtanzania ni mlipa kodi na kila Mtanzania akipata kusoma ndani na nje ya Tanzania ana stahili kupata mkopo. Tutaondoa huo ubaguzi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!