Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu ashinda Urais Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Lissu ashinda Urais Chadema

Spread the love

TUNDU Antipus Lissu, amependekezwa na wajumbe wa Baraza Kuu la Chama cha Demokarsia na Maendeleo (Chadema) kuwa mgombea urais wa chama hicho katika Uchaguzi Mkuu wa Tanzania utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam.

Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye ni John Mnyika, Katibu Mkuu wa Chadema amesema, Lissu amepata kura 405 ya kura zote 442 za wajumbe waliopiga kura leo Jumatatu katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam.

Lazaro Nyalandu ambaye ni mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Kati ambaye amewahi kuwa waziri wa maliasili na utalii, ameshika nafasi ya pili kwa kura 36 na Dk. Mayrose Majinge kura moja.

Amesema jina la Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema Bara litapelekwa kesho Jumanne tarehe 4 Julai 2020 katika mkutano mkuu wa chama hicho kwa ajili ya kuthibitishwa.

Wakati, Mnyika akitangaza matokeo hayo, shangwe zililipuka ukumbini mzima kwa nyimbo na shangwe mbalimbali.

Ikiwa, mkutano mkuu huo utampitisha, Lissu anakwenda kuchuana na mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais John Pombe Magufuli ambaye naye amekwisha kupitishwa na chama chake.

Wagombea wengine wa urais na vyama vyao kwenye mabano ni, Profesa Ibrahim Lipumba (CUF), Hashimu Rungwe (Chaumma) na John Shibuda wa Ade- Tadea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!