Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Tshishimbi, Molinga, Ngassa watemwa rasmi Yanga
Tangulizi

Tshishimbi, Molinga, Ngassa watemwa rasmi Yanga

Spread the love

NAHODHA wa Yanga, Papy Kabamba Tshishimbi pamoja na mshambuliaji raia wa Congo, David Molinga wameachwa rasmi na uongozi wa klabu hiyo mara baada ya mikataba yao kumalizika. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Taarifa iliyotolewa na uongozi wa klabu hiyo imeeleza kuwa jumla ya wachezaji waliochwa ni 14 kutokana na mikataba kuisha na wengine kuvunjiwa mikataba yao.

Wachazaji wengine walioachwa baada ya mikataba yao kumalizika ni Mrisho Ngassa, Tariq Seif na Adrew Vicent.

Kwa upande wa wachezaji ambao watasitishiwa mikataba yao ni pamoja na Patric Sibomana, Yikpe, Eric Kabamba, Jafary Mohamed, Mwalami Issa, Ali Ali na Raphael Daud.

Kwa wachezaji watakaoendelea kusalia kikosini hapo ni Farouk Shikalo, Metacha Mnata, Ramadhan Kabwili, Haruna Niyonzima, Lamine Moro, Said Juma, Juma Mahadhi, Feisal Salum, Adeyum Salehe, Ditram Nchimbi, Deus Kaseke, Mapinduzi Balama, Benard Morrison na Abdulaziz Makame.

Aidha wachezaji Juma Abdul pamoja na Kelvin Yondan ambao mikataba yao imemelizika wapo katika mazungumzo na uongozi huo kwa ajili ya kuendelea kuitumikia klabu hiyo kwa mikataba mipya

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia kutunukiwa udaktari wa heshima Uturuki

Spread the loveBaraza la Chuo Kikuu cha Ankara, ambacho ni cha pili...

error: Content is protected !!