Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Shein: Tujifunze utawala bora kwa Mkapa
Habari za Siasa

Dk. Shein: Tujifunze utawala bora kwa Mkapa

Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein
Spread the love

RAIS wa Zanzibar, Dk. Ali Shein, Rais wa Zanzibar amewataka viongozi wa sasa kujifunza utawala bora kutoka kwa Hayati Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam …. (endelea).

Amesema, Mzee Mkapa aliyefariki usiku wa kuamkia jana tarehe 24 Julai 2020, jijini Dar es Salaam alipokuwa amelazwa tayari ameacha funzo la utawala bora kwa viongozi wa sasa na wajao.

Dk. Shein ametoa kauli hiyo leo tarehe 25 Julai 2020, nyumbani kwa Mkapa, Masaki jijini Dar es Salaam, alipokwenda kuipa pole familia ya rais huyo.

Amesema, viongozi waliopo madarakani wanapaswa kujifunza kutokana na uongozi wa Rais Mkapa, aliyeongoza Tanzania kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.

“Viongozi waliopo madarakani wanapaswa wajifunze kwa marehemu Mkapa, wajifunze uongozi wake. Wale viongozi wa leo tujifunze na amesadifu vizuri. Ameandika kitabu chake,” amesema Rais Shein na kuongeza:

“Tumepata msiba mkubwa kwenye taifa letu na kwa Afrika. Mkapa ni kiongozi wetu, sisi wengine ametulea. Mimi aliniteua Makamu wa Rais, nilifanya naye kazi karibu miaka minne na nusu na nimejifunza mengi,” amesema.

Dk. Sheikn amesema, Mzee Mkapa aliitumikia nchi kwa heshima na nidhamu kubwa, alisimamia misingi ya uchumi wa nchi na maendeleo yake.

Amesema, atamkumba Rais Mkapa kwa mambo mengi ikiwemo uanzishwaji wa utawala bora pamoja na kuleta mageuzi ya kiuchumi.

“Nayakumbuka mengi sana, amesaidia kuibadilisha nchi. Ameanzisha utawala bora, amebadilisha uchumi na alikua wa kwanza kuanzisha Wizara ya Utawala Bora Afrika,” Amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!