Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Serikali ya Tanzania yawahakikishia usalama watalii
Habari Mchanganyiko

Serikali ya Tanzania yawahakikishia usalama watalii

Prof. Adolf Mkenda, Waziri wa Kilimo
Spread the love

WIZARA ya Maliasili na Utalii nchini Tanzania, imewahakikishia usalama wa watalii wanaoingia nchini humo kutembelea utalii hawaathiriki na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu, Kilimanjaro … (endelea).

Kauli hiyo ilitolewa juzi Jumapili tarehe 5 Julai 2020 na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Adolf Mkenda wakati wa uzinduzi wa wimbo uliotungwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro (RC), Anna Mghwira wa kumshukuru Mungu baada ya kumponya corona.

Profesa Mkenda alisema, tayari idadi ya watalii wanaoingia nchini inaongezeka tofauti na ilivyokuwa awali baada ya kuingia ugonjwa wa corona ambao ulisababisha kusitishwa kwa safari katika mataifa mbalimbali.

“Tanzania imechukua hatua kubwa sana na makini katika  kupambana na ugonjwa wa corona na  taratibu zote ambazo zimeelekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) la kuhakikisha usalama wa kila mgeni anayeingia nchini zimefwatwa hivyo tuwaondoe hofu wageni wetu, Tanzania iko salama,” alisema Profesa Mkenda.

Anna Mghwira, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro (katikati)

“Kinachosababisha watalii wasije hapa sio kwamba wanaona tu kwamba huku kuna tatizo lakini kwa nchi zao kuna tatizo.”

“Kwanza wameathirika kiuchumi, wanahofu ya kusafiri kwenda nchi nyingine na wanatoa tahadhari kwa wananchi wao kusafiri wasipokuwa na uhakika kwamba nchi yetu imejipanga vizuri,” alisema Profesa Mkenda

Awali, akizungumzia wimbo huo, RC Anna alisema ameamua kutunga wimbo huo wa shukrani kwa Mungu kwa kumponya na corona baada ya kuambukizwa akiwa katika majukumu ya kuwatumikia wananchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Kengold wakabidhiwa kombe NBC Championship

Spread the loveMdhamini mkuu wa Ligi Daraja la Kwanza (NBC Championship) Benki...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NBC, SILABU waungana kufikisha elimu ya fedha majumbani

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeingia makubaliano ya ushirikiano...

AfyaHabari MchanganyikoMakala & Uchambuzi

Kisukari cha mimba ni nini?

Spread the loveKisukari cha mimba ni aina ya kisukari kinachotokea kwa baadhi...

error: Content is protected !!