Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli: Kupitisha jina ‘inategemea nimeamkaje?’
Habari za Siasa

Rais Magufuli: Kupitisha jina ‘inategemea nimeamkaje?’

Spread the love

RAIS John Magufuli amewataka wateule wake walio na majukumu kutokimbilia majimboni kugombea, na kwamba kupitishwa kwa majina yao kunategemea ‘siku hiyo ataamkaje.’ Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Ametoa tahadhari hiyo leo Jumatatu tarehe 22 Juni 2020, wakati akiwaapisha viongozi wapya wa Mkoa wa Arusha, aliowateua hivi karibuni.

“Ninachotaka kusema sizui kwenda kugombea lakini niwaombe mfikirie zaidi, kama una jukumu lako kubwa unafanya vizuri na watu wanakuamini, itumikie mpaka umalize. Lengo kubwa ni kuijenga Tanzania na kila mmoja anaweza kujenga kokote,” amesema Rais Magufuli.

Amewatahadharisha wateule wake, akisema kwamba, hata kama wakishinda katika kura za maoni ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), anaweza akabatilisha ushindi wao.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo huku akimtolea mfano IGP Simon Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini.

“Lakini nimemteua yeye awe IGP, kaondoka hapa anaenda Bunda na saa nyingine akasema nitamteua kuwa waziri, kwanza hana uhakika kama atashinda kwenye kura za maoni na inawezekana akashinda bado nikamfuta na itatokana siku hiyo nimeamkaje,” amesema Rais Magufuli.

Hata hivyo, Rais Magufuli amesema hawazuii wateule wake kugombea, ila amewataka wajipime ubavu kama wanaweza kushinda katika mchakato wa uteuzi ndani ya CCM.

“Saa nyingine ni kuridhika, hamuwezi mkawa na kila kitu, lakini demokasia iko huru, kama unahakika utashinda nenda kwa spidi kubwa, nafikiri saa nyingine ni kuridhika, kila mahali unaweza kufanya maajabu kwenye nafasi yako,” amesema Rais Magufuli.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!