Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Maofisa 4 NEMC mbaroni tuhuma za utakatishaji fedha
Habari Mchanganyiko

Maofisa 4 NEMC mbaroni tuhuma za utakatishaji fedha

Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inawashikilia watumishi wanne wa Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) kwa tuhuma mbalimbali ikiwemo makosa ya rushwa na utakatishaji fedha. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Watuhumiwa hao, wanashikiliwa katika ofisi za Takukuru, Upanga jijini Dar es Salam na kesho Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 watafikishwa mahakamani.

Taarifa ya Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani aliyoitoa leo Jumatano tarehe 3 Juni 2020 imesema, watuhumiwa hao wamekuwa wakichunguzwa kwa makosa mbalimbali na uchunguzi huo umekamilika.

Amewataja watuhumiwa hao ni; Deusdedith Katwale, Magori Matiku na Obadia Machupa ambao wote ni maafisa mazingira na Lydia Nyinondi ambaye ni Mhasibu Msaidizi. Wote wa makao makuu.

Doreen ametaja tuhuma zao ni; kula njama na kutenda kosa, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuisababishia mamlaka hasara, matumizi mabaya ya madaraka pamoja na utakatishaji wa fedha haramu.

“Tunapenda kuujulisha umma pia, Takukuru kwa kushirikiana na ofisi ya taifa ya mashtaka inatarajia kuwafilisha watuhumiwa hawa mahakamani kesho tarehe 4 Juni 2020,” amesema Doreen

Katikati hatua nyingine, Doreen amesema, Takukuru inamshikilia Eliud Kijalo ambaye ni Afisa wa wizara ya maliasili na utalii kwa makosa ya ubadhirifu wa zaidi ya Sh. 4 bilioni.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yapata tuzo ya mwezeshaji bora wa mikopo serikali Afrika

Spread the loveBenki ya NBC imepata tuzo ya Mwezeshaji Bora wa Pamoja...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

error: Content is protected !!