Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Benki ya TPB, TIB Corparate zaunganishwa
Habari Mchanganyiko

Benki ya TPB, TIB Corparate zaunganishwa

Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kuziunganisha Benki ya TPB na TIB Corparate kuanzia leo tarehe 1 Juni, 2020. Anaripoti Mwandishi, Dodoma … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma leo Jumatatu tarehe 1 Juni, 2020, Msajili wa Hazina nchini Tanzania, Athuman Mbutuka amesema, madeni na mali zote za TIB zitachukuliwa na TPB.

Amesema lengo la kuziunganisha taasisi hizo ni kuongeza ufanisi na kupunguza gharama, “ili kuwa na benki moja imara ya biashara. Muungano huu, utaleta mageuzi mkaubwa ya kiutendaji, muundo na taswira kwa ujumla ili iweze kushindana.”

“Kwa hatua hii tuliyofikia, Benki ya TPB inachukua mali na madeni yote ya iliyokuwa benki ya TIB Corparate na uamuzi huu, umeridhiwa na Benki Kuu ya Tanzania (BoT),” amesema Mbutuka

Amesema, Serikali itaendelea kusimamia utendaji wa benki zote ili  ziimarike kwa maslahi ya wateja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!