Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wagonjwa sita wa corona waongezeka Zanzibar
AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa sita wa corona waongezeka Zanzibar

Hamad Rashid Mohammed, Waziri wa Afya Zanzibar.
Spread the love

WIZARA ya Afya ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imetoa taarifa ya ongezeko la wagonjwa wapya sita (6) wa Corona (COVID-19). Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Kupitia taarifa iliyotolewa leo tarehe 16 Aprili 2020 na Waziri wa Afya visiwani humo, Hamad Rashid inaeleza kuwa idadi hiyo ya wagonjwa inapelekea kufikia idadi ya wagonjwa 24 kutoka 18 ambao waliripotiwa awali ambapo wagonjwa hao watano ni wanaume, mmoja mwanamke na wote ni raia wa Tanzania.

“Wagonjwa wote ni raia wa Tanzania na hawana historia ya kusafiri nje ya nchi siku za hivi karibuni, wote wamelazwa katika vituo maalum kwa ajili ya matibabu,” imeeleza taarifa hiyo.

Wagonjwa hao ni Mwanaume (30) mkazi wa Kibweni, Mwanaume (27) mkazi wa Magogoni, Mwanaume (28) mkazi wa Kwarara, Mwanamke (58) mkazi wa Kilimahewa Juu, Mwanaume (23) mkazi wa Amani na Mwanaume (55) mkazi wa Kidoti.

Aidha, Serikali ya Zanzibar imeendelea kuwasisitiza wananchi kuchukua tahadhari zote za kujikinga na ugonjwa wa Corona na kuwataka wananchi wanaofikwa na misiba mbalimbali kuchukua tahadhari jinsi ya kushughulika na taratibu za mazishi na kuwa wanashauriwa kushirikiana na wataalamu wa afya kwa kupata miongozo sahihi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

Habari Mchanganyiko

GGML yaja na teknolojia za kisasa maonesho ya OSHA Arusha

Spread the loveKATIKA kuelimisha wananchi na washiriki wa maonesho ya usalama na...

error: Content is protected !!