Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Visa vipya 14 vya Corona vyaripotiwa Tanzania
AfyaHabari MchanganyikoTangulizi

Visa vipya 14 vya Corona vyaripotiwa Tanzania

Spread the love

SERIKALI imetangaza ongezeko la  “kesi mpya kumi na nne” (14) za maambukizi ya ugonjwa wa Corona (Covid 19) nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaaam … (endelea).

Taarifa ya wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, iliyosainiwa na waziri wa wizara hiyo, Ummy Mwalimu, imeeleza kuwa wagonjwa wote wapya, ni Watanzania.

“Wizara inatoa taarifa kuwa kuna ongezeko la wagonjwa wapya 14 kutoka 32 waliokuwapo awali,” ameeleza Waziri Ummy na kuongeza, “kati ya hawa wagonjwa 13 wamepatikana Dar es Salaam na mmoja jijini Arusha.”

Amedai kuwa wagonjwa wote hao wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalam wa afya.

Amesema, serikali inaendelea kufuatilia watu waliokaribu na wagonjwa hao na kwamba serikali inaendelea kuwataka wananchi kuepuka misongamano.

Hii ni mara ya kwanza kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kuripoti idadi kubwa ya wagonjwa wa Corona kwa mara moja, tangu kuibuka kwa ugonjwa huo takribani mwezi mmoja uliyopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

Habari Mchanganyiko

Mfanyakazi CRDB atoa sababu za kubambikiwa kesi, hukumu Mei 30

Spread the love  MFANYAKAZI wa Benki ya CRDB, Ibrahim Masahi (40) ameieleza...

Habari Mchanganyiko

Waziri Ummy atangaza Tanzania kuwa kitovu cha utalii tiba

Spread the loveSERIKALI imesema imedhamiria kuifanya Tanzania kuwa kitovu cha matibabu ya...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

error: Content is protected !!