Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea azungumzia siku ya kuhama Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea azungumzia siku ya kuhama Chadema

Saed Kubenea
Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo (Chadema) amesema, siku akitaka kuhama chama hicho, atasaema na si watu kupiga ramli. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Amesema, baadhi ya watu nje na ndani ya Chadema wamekuwa wakimchonganisha na viongozi wa chama hicho, na kwamba hajafikiria kuhama chama hicho kwa sasa.

“Sina mpango huo, sijapanga kuhama. Kama mpango wa kuhama utakuwepo, siku ikifika nitasema,” amesema na kuongeza “watu waache kunichonganisha.”

Kubenea ambaye ni rafiki wa karibu wa Anthony Komu, Mbunge wa Moshi Vijijini (Chadema), aliyetengaza kuhama chama hicho atapomaliza muhula wake, (Kubenea) anahusishwa kuungana naye kutokana na ukaribu wao.

“Urafiki wangu na Komu haimaanishi kila anachofanya nami nakifanya, kwa sababu ya urafiki wangu naye, lakini mpaka sasa hizo ramli ziachwe.

“Mimi bado mbunge wa Chadema Jimbo la Ubungo, ninadhani natakiwa kuendelea kutumikia wananchi wangu.  Waache tufanye kazi, muda ukifika tutazungumza hayo mambo kwa ujumla wake,” amesema Kubenea.

Akizungumzia kuhusu madai hayo, Kubenea amesema yanatokana na vita ya uchaguzi mkuu ujao, hususan kwa watu wanaoliwinda Jimbo la Ubungo.

“Inawezekana ni makundi yanayoibuka kwenye chama hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi. Hakuna mtu anayeweza kufikiri fulani simhitaji.

“Kwa mfano; nispogombea ubunge, mimi nina watu 10,000 katika jimbo nililofanya vizuri, hawawezi wakakupa kura wewe? ” amehoji Kubenea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!