Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto, Wakili wa Serikali wamuibua Azory mahakamani
Habari za SiasaTangulizi

Zitto, Wakili wa Serikali wamuibua Azory mahakamani

Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, amedai kuwa amefurahi kumsikia wakili wa Serikali anakiri kuwa Mwandishi wa habari za uchunguzi, Azory Gwanda amefariki. Anaripoti Mwanandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yameibuka leo tarehe 18 Machi 2020, wakati Zitto akijitetea kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam mbele Hakimu Mkazi Huruma Shaidi. 

Zitto akihojiwa na Nassoro Katuga, Wakili wa Serikali Mwandamizi.

Katuga amemhoji Zitto juu kauli yake lengo la kufanya mkutano wa vyombo vya habari amejibu kuwa lengo ni kuishikiniza Serikali na Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi juu matukio yaliyotokea Mpeta.

Katuga amemuuliza Zitto Juu ya njia za kufikia ujumbe kwa serikali akajibu miongoni mwanzo ni kupitia vyombo vya habari.

Zitto alipoulizwa kwa namna gani wananchi walihusika kwenye ujumbe huo ikiwa alilenga Serikali na jeshi la Polisi liufanyie uchunguzi amejibu kwa mujibu wa katiba Serikali ni ya wananchi hivyo nao wanawajibu wa kupata taarifa.

Wakili wa Serikali alimuuliza Zitto kwanini anashtakiwa kwa kutoa maneno ya uongo akajibu hakushtakiwa kwa kusema maneno ya uongo isipokuwa ameshtakiwa kwa uchochezi ndipo Wakili Katuga akamuuliza kwanini asishtakiwe kwa kueleza habari za kifo cha Ben Saanane au Azory Gwanda Zitto akajibu “Mheshimiwa Hakimu Nimefurahi kusikia Wakili wa Serikali amesema kuwa kweli Azory Gwanda amefariki.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!