Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mabomu yarindima Segerea ‘kwa Mbowe’
Habari za Siasa

Mabomu yarindima Segerea ‘kwa Mbowe’

Spread the love

ASKARI wa Jeshi la Magereza katika gereza la Segerea, wametumia mabomu ya machozi kuwatawanya wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), walikwenda kumsubiri Freeman Mbowe nje ya lango la gereza hilo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Nguvu hiyo ilitumika baada viongozi na baadhi ya wanachama wa Chadema kufika katika gereza hilo, ili kukamilisha taratibu za kumtoa Mbowe.

Viongozi hao wa Chadema walikwenda Segerea baada ya kukamilisha masharti ya faini ya Sh. 70,000,000, hata hivyo walipofika getini, askari hao waliwazuia kuingia.

Kutokana na kuzuiwa, Halima Mdee, Mbunge wa Kawe na viongozi wengine waliokwenda, walishuka kwenye gari ili kusikilizana na askari hao.

Hivyo, wafuasi wa chama hicho waliokuwa eneo hilo, nao walisogea kusikiliza na kushinikiza viongozi wa Chadema waachwe kwenda kukamilisha taratibu za kumtoa Mbowe.

Askari hao walianza kuwapiga na kukamata baadhi ya wafuasi hao, na walipoona hali inazidi kuchafuka, wakalazimika kutumia mabomu ya machozi jambo lililozua taharuki eneo hilo.

Mmmoja kati ya wafuasi alalamika, kuwa licha ya kukamilisha masharti ya kumtoa Mbowe gerezani, bado mamlaka ya gereza hilo inajizungusha kumtoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mpina mwiba CCM, ahofia kuzibwa mdomo

Spread the loveWAKATI Chama cha Mapinduzi (CCM), kikijinasibu kuwa kinara wa demokrasia...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Mabeyo ametuepusha

Spread the loveNIMEGUSWA na uadilifu, utiifu na uaminifu wa Mkuu mstaafu wa...

Habari za SiasaTangulizi

CCM yaitaka TAKUKURU kuichunguza Chadema tuhuma alizoibua Lissu

Spread the loveCHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimeitaka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana...

error: Content is protected !!