Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dk. Bashiru amtisha Membe
Habari za Siasa

Dk. Bashiru amtisha Membe

Spread the love

SIKU mbili baada ya Bernald Membe kusema, uamuzi wa kumkabili Dk. John Magufuli kwenye urais ndani ya chama hicho, ndio uliomfukuzisha, Dk. Bashiru Ally amemtaka wakutane uwanjani. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Dk. Bashiru ambaye ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), amesema ikiwa sababu alizozitoa Membe ndio kilichomfukuzisha kwenye chama hicho, basi ahamie kwenye vyama vingine ili wakutane kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Dk. Bashiru anapingana na hoja ya Membe, kuwa kilichomponza ndani ya chama hicho si hatua zake kuelekea urais, bali utovu wa nidhamu usiovumilika.

Membe alitaka ‘kukomesha’ utamaduni wa CCM kwamba, rais aliyepo madarakani agombee muhula wa pili kupitia chama hicho.

Wiki iliyopita, Membe ambaye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Mbunge wa Mtama, alilieleza gazeti moja la kila siku, kwamba hatua zilizochukuliwa na CCM, zilitokana na kuonesha dhamira ya kumkabili Dk. Magufuli, mwenyekiti wa sasa wa chama hicho katika hatua za kuteuliwa kugombea urais kupitia chama hicho.

Leo tarehe 2 Machi 2020, akiwa katika ofisi za Mwananchi Communication, Dk. Bashiru amemueleza Membe kwamba, Katiba ya CCM haiifungi Katiba ya nchi, na kwamba anaruhusiwa kugombea urais kupitia chama kingine.

“Ukifukuzwa CCM, Katiba haisemi usigombee kwenye vyama 19 vingine,” amesema Dk. Bashiru na kuongeza “ila ukifungwa ndio unaweza ukakosa sifa au ukikwepa kodi, adhabu aliyopewa haihusu sharia za nchi.”

Membe na makatibu wakuu wastaafu wa chama hicho – Abdulrahman Kinana na Yusuf Makamba – waliingia matatani baada ya sauti zao kunaswa zikidaiwa kukejeli uongozi wa chama hicho chini ya Dk. Magufuli

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!