Thursday , 7 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif atikiswa Pemba
Habari za Siasa

Maalim Seif atikiswa Pemba

Maalim Seif Shariff Hamad
Spread the love

AHMED Ngwali, Mbunge wa Wawi mkoani Kusini Pemba kupitia Chama cha Wananchi (CUF), amejivua uanachama na kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Pembe iliyokuwa ngome ya CUF, kwa sasa ni ngome ya Chama cha ACT-Wazalendo ambapo Maalim Seif Sharif Hamad ndio mshauri mkuu wa chama hicho.

Ngwali ametangaza uamuzi huo leo tarehe 2 Machi 2020, katika ziara ya Humphrey Polepole, Katibu wa Itikadi na Uenezi CCM, ya kukagua miradi ya maendeleo visiwani Pemba.

Mwanasiasa huyo amesema, ameamua kujivua uanachama wa CUF pamoja na kujiuzulu ubunge, baada ya kuridhishwa na kasi ya utendaji kazi wa serikali iliyoko madarakani.

“Kwa niaba ya wananchi wa Ziwani leo tarehe 2 Machi 2020, kwa matendo ya CCM mnayofanya naamua kujivua ubunge na kujivua vyeo vyangu vyote vya chama, kuacha kiinua mgongo, kuacha posho za vikao, kwa ajili ya wananchi wetu hawa,” amesema Ngwali.

Ngwali anakuwa mbunge wa kwanza wa upinzani visiwani Zanzibar kuhamia CCM, baada ya sakata hili kushika kasi Tanzania Bara.

Taarifa zaidi zinaeleza, wabunge wengi Pemba wamekuwa watiifu kwa uongozi wa ACT-Wazalendo, huku alama na bendera za CUF zikielekea kutoweka kisiwani humo.

Hata hivyo imeelezwa, wabunge kwenye kisiwa hicho wamekuwa wakishawishiwa kujiunga CCM, kwa ahadi ya ‘kupatiwa’ ubunge kwenye uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bashungwa: Katesh kutafanyiwa usafi wa hali ya juu

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema kazi ya kuondoa tope...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

error: Content is protected !!