Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa: Nakubalika
Habari za Siasa

Mch. Msigwa: Nakubalika

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

MCHUNGAJI Peter Msigwa, Mbunge wa Iringa Mjini, amesema kila baada ya miezi mitatu, hufanya utafiti kubaini idadi ya wananchi wanaomuunga mkono jimboni humo. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam…(endelea).

Mchungaji Msigwa ametoa kauli hiyo alipokuwa kwenye mahojiano na Kituo cha Redio cha East Africa.

Amesema, matokeo ya utafiti anaoufanya yamebaini kwamba kati ya wananchi 10 jimboni humo, saba wanamuunga mkono, wawili wanaunga mkono Chama cha Mapinduzi (CCM), na mmoja hana uamuzi juu ya suala hilo.

Mchungaji Msigwa amesema kufuatia matokeo ya utafiti huo, atagombea tena katika jimbo hilo, kwenye Uchaguzi Mkuu wa Mwezi Oktoba 2020.

“Nagombea,  wananchi wananihitaji bado. Nimekwua na tabia ya kufanya utafiti kila baada ya miezi mitatu . Katika utafiti niliofanya kati ya watu kumi, saba wananiunga mkono, wawili wanaiunga mkono CCM na mmoja hana uamuzi,” amesema Msigwa .

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!