Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Joto Zitto kukamatwa lapanda
Habari za SiasaTangulizi

Joto Zitto kukamatwa lapanda

Zitto Kabwe, Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalando
Spread the love
HATUA ya Zitto Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo kudai kuundiwa zengwe la kuhusishwa na utakatishaji fedha, limekishtua chama hicho. Anaripoti Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Tarehe 7 Februari 2020, akiwa Marekani, Zitto aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter, kwamba anaundiwa mashitaka ya utakatishaji fedha, na kwamba atakaporejea anatakiwa kukamatwa.

“Mpango wa kunishitaki kwa kosa la utakatishaji fedha pindi nitakapotua Dar es Salaam kutoka safari zangu za kimataifa, bado unaendelea,” aliandika Zitto.

Taarifa walizonazo wazee wa chama hicho, zinawatia hofu juu ya mkakati huo ambayo tayari umeelezwa na Zitto mwenyeye ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Mjini.

Leo mbele ya waandishi wa habari, wazee wa cama hicho wakiongozwa na mwenyekiti wao Yassin Mohamed, wamesema mpango huo unalenga kuchochea uovu nchini.

Wameeleza kwamba, Zitto amekuwa akisakamwa ndani naje ya Bunge kutokana na misimamo yake kwa maslahi ya taifa, akitoa mfano wa kuandika barua kwenye Benki ya Dunia (WB), kushinikiza kutotoa fedha za elimu mpaka serikali itakaporuhusu wanafunzi wataopewa mimba, kurejea masomoni.

“Hoja ambayo wanaegemea kuhalalisha matamko hayo ni madai, kwamba Zitto ameisaliti nchi kwa hatua yake ya kuiandikia barua Benki ya Dunia akiomba isitishe mkopo wa elimu nchini, mpaka pale serikali itakapobadili sera yake ya kibaguzi juu ya elimu kwa wanafunzi wa kike, wanaopata mimba wangali shuleni,” amesema Mzee Mohamed.

Mzee Mohamed amesema, hilo haliwezi kukubalika katika nchi ambayo inaheshimu demokrasia na siasa za ushindani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!