Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Virusi vya Corona vyauwa watu 1,000, Watanzania waishio China njiapanda
Habari Mchanganyiko

Virusi vya Corona vyauwa watu 1,000, Watanzania waishio China njiapanda

Watanzania waishio China wakiandamana kuomba kurudishwa nchini
Spread the love

WATANZANIA waishio nchini China,  wako njia panda baada ya kukwama kurejea nchini kufuatia mlipuko hatari wa Virusi vya Corona, vilivyopoteza maisha ya watu zaidi ya 1,000. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Baada ya mlipuko huo kuendelea kuwa tishio, Watanzania hao ambao kwa sasa wamefungiwa sehemu moja ili kunusuru usalama wa maisha yao, wameiomba Serikali ya Tanzania kufanya hima kuwarejesha nchini.

Akizungumzia kuhusu suala hilo, Balozi wa Tanzania nchini China, Mbelwa Kairuki amesema Watanzania hao wako katika wakati mgumu kutokana kwamba, mamlaka nchini China zimeshauri wasisafiri kwenda eneo lolote, ili kukwepa kuambukizwa ugonjwa huo.

Balozi Kairuki amesema uamuzi juu ya maombi ya Watanzania hao kurejeshwa nchini haraka, unatakiwa kuangaliwa kwa umakini kutokana na hali halisi iliyokuwepo, ili kukwepa madhara zaidi.

“Uamuzi utakaofanywa lazima uangalie hali halisi, si busara kufanya maamuzi kwa mihemko. Na tujifunze kwa wenzetu hatua walizochukua na matokeo yake. Ili tusijekuwa na majuto makubwa zaidi,” ameshauri Balozi Kairuki.

Balozi Kairuki ameeleza kuwa, hata nchini Japani Watanzania wote walikuwa wazima, lakini walipoanza kuondolewa, wanafunzi watano walipata maambukizi ya ugonjwa huo, ambao pia waliwaambukiza wenzao watano.

Kutokana na changamoto hiyo, Balozi Kairuki amewataka ndugu, jamaa na marafiki wa wanafunzi hao kumuomba Mungu aendelee kuwalinda, huku akiwahimiza kuwapa moyo wahusika, ili wasikate tamaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!