Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko TCRA: Tumezima laini 975,041, wengine wanafuata
Habari MchanganyikoTangulizi

TCRA: Tumezima laini 975,041, wengine wanafuata

James Kilaba, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)
Spread the love

SERIKALI kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imefunga laini za simu 975,041, zisizosajiliwa kwa mfumo wa alama ya vidole. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Akihojiwa na Televisheni ya Taifa (TBC), Mhandisi James Kilaba, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, amesema laini hizo zilizimwa usiku wa jana tarehe 20 Januari 2020, siku ambayo ilikuwa ukomo kwa watu wasiosajili laini kwa mfumo huo, kukatiwa mawasiliano.

Mhandisi Kilaba ameeleza kuwa, laini hizo zilizofungwa ni za watu wenye namba za vitambulisho vya uraia, vinavyotolewa na Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA).

Amesema, laini hizo zimezimwa kwa makundi, ambapo kundi la kwanza ni laini 656,091 za watu wenye namba za NIDA ambao hawakujisajili, na kundi la pili ni laini 318,950 ambazo usajili wake wa awali ulikuwa na dosari, hivyo zilitakiwa kusajiliwa tena lakini wahusika waligoma kusajili.

“Wenye namba ambao idadi yao kwa ujuma ni 975,041, hawa tutawazimia leo (jana) kuanzia saa 4 usiku, hawa watu wamekuwa wakiitwa lakini hawajarudi. Hawana sababu ya msingi ya kutozimiwa laini zao leo (jana), “ ameeleza Mhandisi Kilaba.

Mhandisi Kilaba amesema, zoezi hilo ni endelevu, na kwamba laini zisizosajiliwa zitazimwa kwa awamu.

“Na baada ya kuzimia hawa, tunazima kidogo kidogo kwa sababu ya mambo ya kiutaalamu, sababu huwezi kuzima laini milioni 5 au 10 kwa wakati mmoja. Watakapoenda wengi zaidi hawawezi kujisajili hawezi kupata huduma,” amesema Mhandisi Kilaba.

Aidha, Mhandisi Kilaba amesema zoezi la usajili wa alama za vidole ni endelevu kwa wale watakaohitaji laini mpya za simu.

“Wewe ambaye unahitaji laini mpya utasajili, usajili haukuwekewa ukomo wa tarehe ya leo, bali uhuishaji wa laini za simu walizokuwa wanamiliki zamani ukomo wao ni leo. Usajili unaendelea kama ambavyo watu watakuwa wanahama kwenda kwenye umri wanaotakiwa kupata simu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!