Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CHAUMMA nao wajiondoa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
Habari za Siasa

CHAUMMA nao wajiondoa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa Chaumma
Spread the love

CHAMA cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), kimetangaza kutoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea). 

Uamuzi huo umetangazwa leo tarehe 9 Novemba 2019 na Hashim Rungwe, Mwenyekiti wa CHAUMMA Taifa, wakati akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam. 

Rungwe ameeleza kuwa, wamejitoa katika uchaguzi huo kwa kuwa mchakato wake ulikuwa na hila, kwa wagombea wa vyama vya upinzani.

“Tunashindwa, tunaona kwamba huu uchaguzi umetayarishwa kwa hila, kwamba wananchi wasishiriki. Tunaona kwamba uchaguzi huu umefanywa hila. Na sisi pia tunaamua hatutashiriki uchaguzi huu. Tunaomba wagombea wetu popote walipo wasishiriki,” ametangaza Rungwe.

Rungwe amesema wamefikia hatua hiyo, baada ya kuona jitihada zao za kutafuta suluhu kuhusu hujuma hizo, kugonga mwamba.

“Wanachama wote wafahamu huu uchaguzi una hila, tumekata rufaa lakini haijasaidia chochote. Kama wao ndio wanataka hivi, kwamba wale wana nguvu, wana dola, sisi hatuko tayari kupigana,” amesema Rungwe na kuongeza;

“Watanzania hatuko tayari kupigana. Hatuna tabia hiyo. Unatuzuia hatufanyi siasa. Sasa uchaguzi halali umeutangaza tumekuja kuchukua fomu, matatizo tunasumbuliwa, tumezirudisha zimekataliwa, tufanye nini.”

Rungwe amesema wananchi ambao ndio wapiga kura, wataamua la kufanya kuhusu uchaguzi.

Rungwe amesema CHAUMMA kilisimamisha wagombea zaidi ya 250, ambapo jiji la Dar es Salaam kilisimamisha wagombea 5, Morogoro (38), Iringa (30), Njombe (20) Tabora (38), Kigoma (10), Mwanza (25), Mara (40), Mtwara (7), Tanga 10 na Shinyanga (6).

CHAUMMA kinakuwa chama cha tatu kuususia uchaguzi huo, baada ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na ACT- Wazalendo, kutangaza kujiondoa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!