Saturday , 4 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Ebola: Tanzania yaishangaa WHO
Afya

Ebola: Tanzania yaishangaa WHO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeeleza kushangazwa na kauli ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwamba ilikugoma kutoa taarifa kuhusu kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola. Anaripoti Faki Sosi … (Endelea).

“Sisi wenyewe tumeshangaa kwanini WHO (Shirika la Afya Duniani) wametoa taarifa ya kwamba hatujawapa sampuli? Sisi tunashangaa kwanini wametoa hiyo taarifa lakini nyie wenye ni mashahidi, mwakilishi wa WHO alisema kwamba hakuna Ebola Tanzania,” amesema Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya leo tarehe 3 Oktoba 2019.

Amesema, Tanzania hakuna ugonjwa wa Ebola na kwamba hakuna mtu yeyote aliyebainika kuwa na ugonjwa huo.

Waziri Ummy amesema, kwa sasa ugonjwa huo upo Kaskazini  mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Na kwamba, kwa kuwa DRC ipo jirani na Tanzania, serikali imeanza kuchukua za tahadhari huku akisisitiza, taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao kuhusu uwepo wa ugonjwa huo nchini, hazina ukweli wowote.

“Kipaumbele chetu sisi baadala ya tuhuma na kutoaminiana kwamba tunaficha taarifa, tumeweka wataalamu kwenye mipaka,” amesema na kwamba, mipaka yote iliyokuwa rasmi na ile ambayo sio rasmi, imedhibitiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

200 wapimwa afya na GGML katika maonesho ya OSHA

Spread the loveZAIDI ya watu 200 jijini Arusha wamejitokeza kupimwa afya na...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

AfyaHabari Mchanganyiko

Songwe katika mikakati ya elimu ya lishe kudhibiti udumavu

Spread the love  SERIKALI mkoani Songwe imejipanga kuendelea kutoa elimu ya lishe...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

error: Content is protected !!