Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Michezo Simba wang’ara tuzo za mwezi VPL
Michezo

Simba wang’ara tuzo za mwezi VPL

Spread the love

KOCHA mkuu wa klabu ya Simba Patrick Aussems na mshambuliaji wake, Miraji Athuman wameibuka vinara wa tuzo za mwezi Septemba za Ligi Kuu Tanzania Bara 2019/20. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Miraji amefanikiwa kushinda tuzo hiyo baada ya kumshinda tuzo ya mchezaji bora wa mwezi, baada ya kuwashinda mwenzake wa klabu ya Simba Meddy Kagere na Ismail Kada kutoka Tanzania Prisons, wakati Aussems ameshinda tuzo ya kocha bora baada ya kuwabwaga makocha Mohammed Rishard wa Prisons na Abdallah Mohammed Baresi wa JKT Tanzania.

Aussems amefanikiwa kushinda tuzo hiyo baada ya kufanikiwa kuingoza Simba kushinda michezo minne ya Ligi Kuu Tanzania Bara na kufanikiwa kukusanya jumla ya pointi 12 na kufanya timu hiyo kuwa kileleni kwenye msimamo wa ligi hiyo.

Kwa upande wa Miraji ameshinda tuzo hiyo baada ya kuwa katika kiwango kizuri kwa kufanikisha timu yake kupata ushindi mbele ya Mtibwa Sugar baada ya kufunga bao la pili sambamba na kutoa pasi mbili za mabao na hivyo atazawadiwa kiasi cha Sh. 1,000,000 kutoka kwa mdhamini wa mkuu wa Ligi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Meridianbet yaibukia Tandika, yafungua duka jipya

Spread the love BAADA ya kupita maeneo mbalimbali hatimae kampuni yaMeridianbet imeibukia...

BiasharaMichezo

Ukiwa na Meridianbet ni rahisi kuwa milionea

Spread the love  CARABAO Cup raundi ya 3 Uingereza inaendelea na mechi...

Michezo

Jezi ya Samatta iliyoifunga Liverpool kuuzwa Genk

Spread the love  KLABU ya KRC Genk ya nchini Ubelgiji imeamua kuanza...

BiasharaMichezo

Hii ndio historia ya El-Clasico, derby bora zaidi duniani

Spread the love  KILA nchi ina vilabu viwili hasimu na pinzani nje...

error: Content is protected !!