Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Afya Ebola: Tanzania yaishangaa WHO
Afya

Ebola: Tanzania yaishangaa WHO

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu
Spread the love

SERIKALI ya Tanzania imeeleza kushangazwa na kauli ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kwamba ilikugoma kutoa taarifa kuhusu kuwepo kwa ugonjwa wa Ebola. Anaripoti Faki Sosi … (Endelea).

“Sisi wenyewe tumeshangaa kwanini WHO (Shirika la Afya Duniani) wametoa taarifa ya kwamba hatujawapa sampuli? Sisi tunashangaa kwanini wametoa hiyo taarifa lakini nyie wenye ni mashahidi, mwakilishi wa WHO alisema kwamba hakuna Ebola Tanzania,” amesema Ummy Mwalimu, Waziri wa Afya leo tarehe 3 Oktoba 2019.

Amesema, Tanzania hakuna ugonjwa wa Ebola na kwamba hakuna mtu yeyote aliyebainika kuwa na ugonjwa huo.

Waziri Ummy amesema, kwa sasa ugonjwa huo upo Kaskazini  mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Na kwamba, kwa kuwa DRC ipo jirani na Tanzania, serikali imeanza kuchukua za tahadhari huku akisisitiza, taarifa zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao kuhusu uwepo wa ugonjwa huo nchini, hazina ukweli wowote.

“Kipaumbele chetu sisi baadala ya tuhuma na kutoaminiana kwamba tunaficha taarifa, tumeweka wataalamu kwenye mipaka,” amesema na kwamba, mipaka yote iliyokuwa rasmi na ile ambayo sio rasmi, imedhibitiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the loveTIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini...

Afya

Wananchi 530,000 kufaidika na ujenzi wa hospitali ya bil. 1.8

Spread the love  SERIKALI imetoa Sh 1.8 bilioni kwa ajili ya ujenzi...

error: Content is protected !!