Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wizara Viwanda, Kilimo washirikiane – Mhandisi Manyanya
Habari Mchanganyiko

Wizara Viwanda, Kilimo washirikiane – Mhandisi Manyanya

Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Spread the love

WIZARA ya Viwanda na Biashara lazima ishirikiane na Wizara ya Kilimo ili kuleta tija kwa wakulima na wafugaji. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Mhandisi Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara leo tarehe 7 Agosti 2019 alipotembelea maonyesho ya wakulima na wafugaji Kanda ya Kati katika viwanja ya Nzuguni, Dodoma.

Amesema, wakulima na wafugaji wanatakiwa kufundishwa matumizi ya teknolojia ya kisasa, waweze kufuga na kulima kisasa ili walete tija zaidi na kuongeza kipato.

“Awali wakulima walitekelezwa, lakini sasa tunasisiza zaidi makundi mbalimbali yakiwemo ya wakulima na wafugaji, yashirikishwe kufanya kazi zao kwa tija,” amesema Mhandisi Manyanya.

Amesema, wananchi wanaweza kufundishwa kutumia teknolojia rahisi katika kusindika mazao kama vile nyanya na mazao mengine, ili yasiharibike badala ya kufikiria kuwa na viwanda vikubwa ambayo siyo rahisi wajasiriamali wadogo kuvipata.

“Naona bado kuna changamoto kwa wajasirimali wadogowadogo, maeneo ya kufanyia biashara siyo rafiki kwao. Wengi wanafanyia shughuli zao juani, ni vyema wakapatiwa maeneno mazuri ili wafanye kazi zao vizuri zaidi na kuwaletea tija,” amesema Mhandisi Manyanya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!