Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Z’bar: Wachanganya juisi na dawa nguvu za kiume, wakamtwa
Habari Mchanganyiko

Z’bar: Wachanganya juisi na dawa nguvu za kiume, wakamtwa

Juisi ya tende
Spread the love

HAMID Hemed Salum (39) na Saidi Hemed Salum (40) wamekamatwa na Wakala wa Dawa, Chakula  na Vipodozi Zanzibar (ZDFA), kwa tuhuma za kuuzia wateja juisi ya tende iliyochanganywa na dawa za kuongeza nguvu za kiume kisiwani Unguja. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumzia kuhusu sakata hilo, Nassir Ali Buheti, Kaimu Mkurugenzi wa Wakala wa Dawa, Chakula  na Vipodozi Zanzibar (ZDFA) amesema, wamekamatwa na maofisa wa wakala huo, baada ya kubainika kuuza juisi hiyo kwa zaidi ya miezi sita.

Buheti ameeleza kuwa, baada ya ZDFA kupata tetesi za watuhumiwa hao kuuza juisi ya tende yenye dawa za kuongeza nguvu za kiume, wakala huo ulituma ofisa wake kwa ajili ya kufanya uchunguzi.

“Nilipata taarifa kwamba kuna mfanyabaishara anafanyabiashara katika gari, anauza juisi ya tende lakini pia anauza dawa ya kuongeza nguvu za kiume,” amesema Buheti.

Amesema, baada ya ofisa wake kufika eneo la wafanyabishara hao, aliuziwa juisi ya tende iliyochanganywa na dawa ya kuongeza nguvu za kiume.

“Tulituma ofisa wetu kwa ajili ya kuchunguza, akauziwa juisi ya tende iliyo na dawa ya kuongeza nguvu za kiume na kupewa namba kama akihitaji tena,” amesema Buheti.

Amesema, kitendo kilichofanywa na wafanyabiashara hayo ili kuvutia wateja, ni hatari kwa afya ya binaadamu.

Mtuhumiwa Salum amesema, dawa hizo huchukua kutoka kwenye maduka la dawa akitaja kuwa ni Viagra na kuzichanganya katika juisi hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!