Sunday , 19 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif arejea nyumbani kwake
Habari za Siasa

Maalim Seif arejea nyumbani kwake

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, mshauri mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, aliondoka kwenye Kongamano la Kuadhimisha Miaka 9 ya Maridhiano visiani humo na kurejea nyumbani kwake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa za awali zilieleza, mwanasiasa huyo mkongwe na mwiba kwa Serikali ya Rais Mohammed Shein na Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo, alikwenda polisi kuitikia wito.

Ni baada ya ujumbe wa Jeshi la Polisi kumtaka aende kwa ajili ya mahojiano. Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuondoka kwenye kongamano hilo, Maalim Seif alikwenda moja kwa moja nyumbani kwake.

Kwenye kongamano hilo, Maalim Seif aliondoka huku akisindikizwa na baadhi ya polisi jambo ambalo liliashiria kwenda kuitikia wito huo.

Maalim Seif ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Pili wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), alihudhuria konagamano hilo lililoandaliwa na Mzee Nassoro Moyo, mwanasiasa mkongwe visiwani humo.

Kongamano hilo lilisimamishwa saa 6 mchana kwa agizo la Jeshi la Polisi. Hata hivyo, polisi walidai muda wa kongamano hilo ulikwisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Wakili Mwabukusi anusurika kufungiwa, asema hatarudi nyuma

Spread the loveWAKILI Boniface Mwabukusi amesema kuwa hatorudi nyuma kuwatetea Watanzania na...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RC Chongolo atangaza ‘vita’ kwa wanaovusha wageni kinyemela

Spread the loveKATIKA kulinda usalama wa nchi kupitia mpaka wa Songwe, Mkuu...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

RUWASA yachongewa, yateketeza mamilioni kwa maji yenye magadi

Spread the loveSAKATA la ukosefu wa maji wilayani Momba mkoani Songwe limezidi...

Habari MchanganyikoHabari za SiasaTangulizi

Lissu akabidhiwa gari lake, aomba msaada wa matengenezo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu leo Ijumaa amekabidhiwa...

error: Content is protected !!