Friday , 29 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif arejea nyumbani kwake
Habari za Siasa

Maalim Seif arejea nyumbani kwake

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, mshauri mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, aliondoka kwenye Kongamano la Kuadhimisha Miaka 9 ya Maridhiano visiani humo na kurejea nyumbani kwake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa za awali zilieleza, mwanasiasa huyo mkongwe na mwiba kwa Serikali ya Rais Mohammed Shein na Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo, alikwenda polisi kuitikia wito.

Ni baada ya ujumbe wa Jeshi la Polisi kumtaka aende kwa ajili ya mahojiano. Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuondoka kwenye kongamano hilo, Maalim Seif alikwenda moja kwa moja nyumbani kwake.

Kwenye kongamano hilo, Maalim Seif aliondoka huku akisindikizwa na baadhi ya polisi jambo ambalo liliashiria kwenda kuitikia wito huo.

Maalim Seif ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Pili wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), alihudhuria konagamano hilo lililoandaliwa na Mzee Nassoro Moyo, mwanasiasa mkongwe visiwani humo.

Kongamano hilo lilisimamishwa saa 6 mchana kwa agizo la Jeshi la Polisi. Hata hivyo, polisi walidai muda wa kongamano hilo ulikwisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!