Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Maalim Seif arejea nyumbani kwake
Habari za Siasa

Maalim Seif arejea nyumbani kwake

Spread the love

MAALIM Seif Sharif Hamad, mshauri mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, aliondoka kwenye Kongamano la Kuadhimisha Miaka 9 ya Maridhiano visiani humo na kurejea nyumbani kwake. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Zanzibar … (endelea).

Taarifa za awali zilieleza, mwanasiasa huyo mkongwe na mwiba kwa Serikali ya Rais Mohammed Shein na Chama Cha Mapinduzi (CCM) visiwani humo, alikwenda polisi kuitikia wito.

Ni baada ya ujumbe wa Jeshi la Polisi kumtaka aende kwa ajili ya mahojiano. Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuondoka kwenye kongamano hilo, Maalim Seif alikwenda moja kwa moja nyumbani kwake.

Kwenye kongamano hilo, Maalim Seif aliondoka huku akisindikizwa na baadhi ya polisi jambo ambalo liliashiria kwenda kuitikia wito huo.

Maalim Seif ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Pili wa Rais katika Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), alihudhuria konagamano hilo lililoandaliwa na Mzee Nassoro Moyo, mwanasiasa mkongwe visiwani humo.

Kongamano hilo lilisimamishwa saa 6 mchana kwa agizo la Jeshi la Polisi. Hata hivyo, polisi walidai muda wa kongamano hilo ulikwisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!