Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa azindua safari za treni ya mizigo Tanga-Moshi
Habari Mchanganyiko

Majaliwa azindua safari za treni ya mizigo Tanga-Moshi

Spread the love

KASSIM Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amezindua safari za treni za mizigo kutoka Mkoa wa Tanga kuelekea Kilimanjaro. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 20 Julai 2019 katika viwanja vya Stesheni ya Moshi, mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Majaliwa amesema utekelezaji wa urejeshaji huduma ya usafiri wa reli nchini, ni muendelezo wa jitihada za serikali katika kufikisha huduma muhimu kwa jamii.

Majaliwa amesema serikali itaanzisha usafiri wa treni ya abiria kutoka Dar es Salaam, Moshi hadi Arusha.

“Tunaendelea kuboresha miundombinu ya reli ili kuifungamanisha na sekta nyingine, ndiyo maana tumewekeza katika ujenzi wa reli ya kisasa na ukarabati wa reli ya kati. Tutaanzisha Usafiri wa treni ya abiria kutoka Dar-Moshi-Arusha,” amesema Majaliwa.

Masanja Kadogosa, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania (TRC) amesema serikali imetumia Sh. 5.7 bilioni kuirudisha njia hiyo, iliyofungwa kwa miaka 12.

“Mpaka sasa tumetumia Sh. 5. 7 bilioni kuirudisha njia hii, na wahandisi wazawa ndio wamesimamia zoezi hili lote,” amesema Kadogosa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Biteko aipongeza GGML kudhibiti vifo, majeruhi mahali pa kazi

Spread the loveNAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

error: Content is protected !!