CHAMA cha ACT-Wazalendo kupitia ngome yake ya wazee, kimetoa msimamo kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Akizungumza na wanahabari leo tarehe 6 Julai 2019, Yeremia Maganja, Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ACT-Wazalendo, amesema chama hicho kitashirikiana na vyama vingine vya siasa, ili kuhakikisha vyama vya upinzani vinanyakua ushindi kwenye uchaguzi huo.
Maganja ameeleza mikakati ya ushindi katika uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha mazingira ya uchaguzi huru na wa haki yanakuwepo, ikiwemo upatikanaji wa Tume Huru ya Uchaguzi.
Amesema kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi kutasaidia kuondoa changamoto ya ukiukwaji wa misingi ya katiba na sheria, katika mchakato wa uchaguzi.
Wajumbe wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo kutoka mikoa mbalimbali wamekutana leo jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya kushiriki katika kikao cha kikosi kazi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019.
Leave a comment