Tuesday , 30 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee ACT-Wazalendo watoa neno maandalizi uchaguzi 2019
Habari za Siasa

Wazee ACT-Wazalendo watoa neno maandalizi uchaguzi 2019

Bendera ya ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kupitia ngome yake ya wazee, kimetoa msimamo kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 6 Julai 2019, Yeremia Maganja, Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ACT-Wazalendo, amesema chama hicho kitashirikiana na vyama vingine vya siasa, ili kuhakikisha vyama vya upinzani vinanyakua ushindi kwenye uchaguzi huo.

Maganja ameeleza mikakati ya ushindi katika uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha mazingira ya uchaguzi huru na wa haki yanakuwepo, ikiwemo upatikanaji wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Amesema kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi kutasaidia kuondoa changamoto ya ukiukwaji wa misingi ya katiba na sheria, katika mchakato wa uchaguzi.

Wajumbe wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo kutoka mikoa mbalimbali wamekutana leo jijini Dar es Salaam,  kwa ajili ya kushiriki katika kikao cha kikosi kazi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!