Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee ACT-Wazalendo watoa neno maandalizi uchaguzi 2019
Habari za Siasa

Wazee ACT-Wazalendo watoa neno maandalizi uchaguzi 2019

Bendera ya ACT-Wazalendo
Spread the love

CHAMA cha ACT-Wazalendo kupitia ngome yake ya wazee, kimetoa msimamo kuhusu ushiriki wake katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 6 Julai 2019, Yeremia Maganja, Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ACT-Wazalendo, amesema chama hicho kitashirikiana na vyama vingine vya siasa, ili kuhakikisha vyama vya upinzani vinanyakua ushindi kwenye uchaguzi huo.

Maganja ameeleza mikakati ya ushindi katika uchaguzi huo, ikiwemo kuhakikisha mazingira ya uchaguzi huru na wa haki yanakuwepo, ikiwemo upatikanaji wa Tume Huru ya Uchaguzi.

Amesema kupatikana kwa Tume Huru ya Uchaguzi kutasaidia kuondoa changamoto ya ukiukwaji wa misingi ya katiba na sheria, katika mchakato wa uchaguzi.

Wajumbe wa Ngome ya Wazee ya ACT-Wazalendo kutoka mikoa mbalimbali wamekutana leo jijini Dar es Salaam,  kwa ajili ya kushiriki katika kikao cha kikosi kazi kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!