Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mali za Mbowe zapigwa mnada kufidia deni la Bil. 1
Habari MchanganyikoTangulizi

Mali za Mbowe zapigwa mnada kufidia deni la Bil. 1

Baadhi ya vifaa Bilicanas iliyokuwa inamilikiwa na Freeman Mbowe
Spread the love

BAADHI ya vifaa vya Kampuni ya Mbowe Limited (Bilicanas) vimepigwa mnada leo tarehe 6 Julai 2019 na Kampuni ya Udalali ya Fosters Auctioneers & General Traders ya jijini Dar  es Salaam. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Mnada huo umefanyika leo chini ya Joshua Mwaituka, dalali wa mahakama, kwenye ghala la Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) lililopo maeneo ya Bandarini, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kuhusu mnada huo, Mwaituka amesema mwitikio wa wateja umekuwa mzuri, na kwamba asilimia kubwa ya vifaa hivyo vimepata wateja.

“Vitu karibu vyote vimeuzwa, kasoro makochi, bei ni za kawaidia. Mwitiko wa watu ni mzuri wamekuja tangu saa 2 asubuhi, kuna waliondoka lakini hao waliobaki wakasema bora wanunue,” amesema Mwaituka.

Mwaituka ametaja baadhi ya vifaa vilivyopigwa mnada ikiwemo, taa ambazo mteja wa mwisho alifikia bei kiasi cha Sh. 7 milioni, jukwaa (Sh. 5.1 milioni), viti, kreti za bia, genereta, mashine ya kupozea (Cooling System) na samani mbalimbali.

Japhet Mwanasenga, Meneja wa Ukusanyaji Madeni kutoka NHC amesema mnada huo ni muendelezo wa shirika hilo katika kudai deni la zaidi ya Sh. 1 bilioni, kutoka kwa kampuni ya Mbowe Limited (Bilcanas) inayomilikiwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa.

Mwanasenga amesema NHC ilichelewa kupiga mnada mali hizo, kutokana na mmiliki wake (Mbowe) kufungua kesi mahakamani ya kuzuia mali zake kuuzwa.

Aidha, Mwanasenga amesema fedha zitakazopatikana kupitia mnada huo, zitaingizwa katika deni la kampuni hiyo, na kwamba kiasi cha deni kitakachosalia, wahusika watalipa kwa mujibu wa sheria.

“Tulikuwa tunamdai Sh. 1.1 bilioni. Tutatumia taratibu zote zikikamilika tutamjuza kiasi tulichouza, kilichobaki lazima alipe,” amesema Mwanasenga na kuongeza.

“Vitu vilichelewa kuuzwa kwa sababu mbowe alienda kupinga mahakamani kutouziwa vyombo vyake, akashindwa kesi tukauza.”

Vifaa vilivyopigwa mnada ambavyo vilikuwa vinatumika katika klabu ya usiku ya Bilicanas,  vilichukuliwa na NHC Mwezi Septemba mwaka 2016, baada ya mmiliki wake kushindwa kulipa deni la zaidi ya Sh. 1 bilioni.

Deni hilo limetokana na malimbikizo ya kodi, ambapo Mbowe kupitia kampuni yake alikuwa mpangaji katika jengo la NHC lililoko makutano ya mitaa ya Mkwepu na Indira Ghandi katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

error: Content is protected !!